UNAFIKI WA VIONGOZI WA KISIASA KAMA MKAKATI WA KUWAWEKA MAMLAKANI: MFANO KUTOKA RIWAYA ZA KATAMA MKANGI: MAFUTA NA WALENISI
Requires Subscription PDF (Swahili)

How to Cite

UNAFIKI WA VIONGOZI WA KISIASA KAMA MKAKATI WA KUWAWEKA MAMLAKANI: MFANO KUTOKA RIWAYA ZA KATAMA MKANGI: MAFUTA NA WALENISI. (2024). JARIDA LA CHAUKIDU. https://doi.org/10.0255/6jykby19

Share

Abstract

Makala haya yanaangazia usawiri wa unafiki wa viongozi wa kisiasa kama
mkakati wa kuwaweka mamlakani katika riwaya za Katama Mkangi Mafuta na
Walenisi. Riwaya zote mbili ni za kiitikadi. Zinachunguza jinsi mfumo wa kisiasa
unaodhibitiwa na tabaka la wachache unavyoweza kuathiri maisha ya
wanaotawaliwa kisiasa. Riwaya hizi zinaonesha uovu uliopo katika tawala ambazo
hazitilii maanani masilahi ya wanyonge. Ni kielelezo cha jinsi jamii inavyoweza
kujinasua kutoka katika mfumo unaowakandamiza na unaowadhalilisha wengi.
Mkangi amesawiri viongozi dhalimu wa kibepari wanaojiweka na kujisetiri
mamlakani kupitia unafiki. Makala haya yanadhamiria kusawiri madhila
wanayotendewa wanajamii na viongozi dhalimu wasiowajali kupitia unafiki ambao
wameufanya kuwa ukweli. Kilele cha uozo wa viongozi wa kisiasa kinajitokeza
wakati ambapo uhuru wa kuongea unadhibitiwa na yeyote anayepatikana na ‘hatia’
hii anahukumiwa kifo au anapata adhabu ya kufutwa kazi pasipo na sababu yenye
mashiko. Jitihada za wanyonge za kukata silisili za udhalimu zinabainika
wanapoamua kupindua mfumo huu wa kisiasa kwa kuwatimua viongozi dhalimu
na wanafiki kupitia mapinduzi. Umuhimu wa makala haya ni kubainisha kuwa
kupitia kazi za sanaa, hasa fasihi andishi, msomaji anaweza kubaini hali halisi ya
maisha yake na wakati huohuo kupata suluhu ya kutatua matatizo yanayomkumba
na jamii yake.

Requires Subscription PDF (Swahili)
Creative Commons License

This work is licensed under a Creative Commons Attribution 4.0 International License.

Copyright (c) 2024 JARIDA LA CHAUKIDU

Downloads

Download data is not yet available.